KIPPRA

KIPPRA

An International Centre of Excellence in Public Policy and Research

AJENDA YA MAGEUZI YA VIJANA TANGU UHURU WA NCHI HADI MAKADIRIO YA SIKU ZA USONI

Ajenda  ya  mageuzi  ya  vijana  tangu  uhuru  imekuwa  ya  kuungwa  mkono,  kufundisha  maadili,  ulengaji  mahiri  wa  kiufundi, utendaji  wa  mikakati,  mawasiliano  na  ubia  madhubuti.

Maendeleo  na  juhudi  za  kuimarika  zimekuwepo,  zipo  na  bado  zitakuwepo.  Kiufupi  nchi imepiga  hatua  Kwa  asilimia  kubwa  kwa  ajenda  ya  mageuzi  ya  vijana  tangu  tangu  kupata  uhuru.

Kwa  mazingira  ya  kawaida  kuna  maendeleo  mengi  mno  juu  ya  mageuzi  ya  vijana. Kwanza  nchi  imejikita  katika  mwendelezo  mzuri  wa  elimu  kwa  vijana  kutoka  kwa   wale  wenye  umri  mdogo mpaka  kwa  wale  ambao  wamebalehe  na  kukomaa. Pili  ni  kuwa  vijana  wanapoikumbatia  elimu  ya  upili  (sekondari)  walimu  huanza  kuwapa  wasia  kuhusiana  na  maisha  pamoja  na  masomo  yao. Hapa  ndipo  vijana  wengi  hupewa  maelezo  juu  ya  mstakabali  wa kuchangua  ‘kozi’  ambazo  watafanya  vyuoni. Hawaambiwi  tu  uzuri  wa  masomo  fulani  vyuoni  ila  pia  huelezewa  manufaa  ya  masomo  hayo  maishani  mwao.

Kutokana  na  serikari  kuwekeza  katika  mazingira  ya  elimu  kwa  kukarabati  au  kujenga  miundo  mbinu, maendeleo  kwenye  ajenda  ya  mageuzi  ya  vijana  yameimarika.

Ufadhili  wa  vijana  katika  masomo  yao  kwenye  vyuo  vya  anuai  na  vyuo  vikuu  ni jambo  ambalo  serikali  imewekeza  kwa  asilimia  kubwa  ili  kutimiza  ajenda  ya  mageuzi  ya  vijana. Kwa  serikali  kuu  imekuwa  wajibu  kwani  isipozifadhili  shughuli  za  vijana  masomoni  makadirio  yao  ya  siku  za  usoni  yatafeli. Hii   ni  kupitia  ufadhili  wa  HELB, ‘Capitation’ pamoja  na  basari  zinazopeanwa  na  viongozi  wa maeneo  bunge, wadi  pamoja  na  magavana katika  sehemu  husika.Serikali imekuwa ikishirikiana na mashirika ya kibinafsi ili kutoa ufadhili wa elimu ya ziada ndani na nje ya nchi kwa vijana walio na uwezo wa kubuni vitu tofauti tofauti. Wapo  baadhi  ya  vijana  ambao huchuma tonge  kubwa  kwa  uvumbuzi  na ubunifu  wao   kwa juhudi  za  kufadhili  kimasomo  zaidi   na  serikali.

Serikali ya Kenya imeweka sera za kuhakikisha ajenda ya mageuzi ya vijana inafanikishwa.Hii ni kupitia kuwapa nafasi za uongozi serikalini ili kuwapevua macho na kuwathamini kwa shughuli tofauti kwa lengo la kukuza viongozi wa baadaye.Kupitia nafasi hizi adhimu serikali inaimarisha ajenda za mageuzi za vijana. Na  shughuli  za  vijana  uongozini  nchini  zimeongezeka  mno  kushinda  awali. Asilimia  kubwa  ya  vijana  imejikita  katika  kugombea nyadhifa  mbalimbali  za  uongozi  katika  siasa  za  nchi  hii  tukufu. Pia  serikali  imeanzisha  mashirika  ya  kuwafunza  vijana  adabu  pamoja  na kazi  zingine  nyingi  ambazo  zina  manufaa  kemkem. Lipo  shirika  la  National  youth  service(NYS)  ambalo  limetengwa  mahsusi  kwa vijana  kuweza  kufanyishwa mazoezi  na  baada  ya  miezi  sita hupelekwa vyuoni  ama  vyuo  vya  anuai  kusomea  kozi  ambazo  wanazipendelea. Hii imeimarisha  nidhamu  kwa  vijana  wengine  nchini. Wengi  wametimiza  ndoto  zao  kupitia  shirika  hili.

Aidha  serikali  imependekeza sera  zipangwe   kwa  kuzingatia  matakwa  ya  vijana  kuanzia  ngazi  ya  kitaifa  hadi  mashinani, pia  kuna  sera  za  kubuni  pragramu  zinazolenga  vijana  katika  maeneo  wanayoishi  ili  kutambua  haki  za  vijana  na  maendeleo  yao  kwa  kuzingatia kwamba  wana  ndoto  zao  ambazo wangependa  kutimiza.

Serikali inatumia takwimu za sasa na kutumia ujuzi wa vijana na uzoefu wao katika kupanga,kutekeleza na kutathmini sera za vijana.Ujuzi wa vijana hutumiwa kwingi sana nchini.Wapo vijana ambao ni wazuri mno katika shughuli za kupanga na kupamba majukwaa ya matamasha.Matamasha hayo huwapa  vijana ajira kwingi nchini.Wapigaji picha kwenye hayo matamasha asilimia kubwa huwa ni vijana.Hii pia hupigiwa mfano,vijana wanapoteuliwa kujiunga na jeshi la nchi.Wengi huwekwa mahali salama kulingana na talanta zao au ubunifu wao.Wapo ambao watapelekwa kwenye taaluma ya kupika jeshini.Wengine huingia jeshini kama madereva n.k.

Mathalani vijana wengi ni walioko vyuoni wengi wao huwa hawana muda wa kujihusisha na mambo yanayowahusu.Kwao huona ni kupoteza muda.Serikali pia imeweka kitengo cha pesa taslimu kwa maendeleo ya vijana ila vijana hawashughuliki kabisa  na manufaa  ya  hizo  fedha.

Ijapokuwa  serikali  inapambana  mno  kufanikisha  ajenda  ya  mageuzi  ya  vijana. Kutimiza  na  kuzingatia  matakwa  ya  sera  walizoziweka  umekuwa  mtihani  mgumu  sana. Sera  za  kuwapa  vijana asilimia  kubwa  kwenye  ajira  ya  kazi  za  serikalini  umekuwa  mtihani  haswa! Kama  sio  mtihani  basi  donda ndugu  ambalo  halisikii  dawa  kabisa.

Jambo  jingine  ambalo  linazuia  maendeleo  katika  ajenda  ya  mageuzi  ya  vijana  ni  dawa  za  kulenya. Vijana  wengi  wamejikita  kwenye  matumizi  ya  dawa  za  kulevya  kutokana  na  shinikizo  kutoka  kwa  vijana  wenzao ,uraibu  na  kukosa  cha  kufanya. Hizi  dawa  za  kulevya  huwapotezea  muda  wao  muhimu  ambao  wanaweza  kuutumia  kufanikisha  ajenda  ya  mageuzi kwa  vijana  nchini.

Aidha  vijana  wengi  wanapenda  kutumia  muda  wao  mwingi  kwenye  mitandao  ya  kijamii  pasi  na  upangaji  mzuri  wa  mikakati  yao  juu  ya  mambo  ya msingi  maishani  mwao. Ili  kukuza  na  kupata  maendeleo  endelevu  katika  ajenda  ya  mageuzi  ya  vijana  nchini  siku  za  usoni. Serikali  inafaa  kuwekeza  mno  katika  masuala  yenye  faida  kwenye  mitandao  ya  kijamii  kwa  kuwa  vijana  wengi  wametekwa  na  mitandao.

Serikali pia inafaa kuweka njia mwafaka za  kuweza  kutimiza  sera  ambazo  inaweka  katika  ajenda  za  mageuzi  ya  vijana. Sera  nyingi  zinazowekwa  hazifatiliwi. Kando  na hayo  serikali  inafaa  kufungua  vituo  vingi zaidi vyenye  manufaa  kwa  nchi  na   kwa  vijana  kwa mafunzo   mahsusi  katika  idara  zote  za  kazi nchini. Kwa  kufanya  hivyo  vijana  wengi  watajitambua  na  watakuwa  na  uwezo  wa kuchapa  kazi  tofauti  tofauti  bila  kulia  eti hakuna  kazi  kwa  vijana  nchini.

Mhandishi: Agadias  Ikoha  Yambasa, Mwanafunzi, Sigalagala National Polytechnic

Share this post

Stay Up to Date

More Blogs